Ukweli Wa Aganao Na Ibrahimu

hft swahili 2022
Hope for Today (Swahili)
Ukweli Wa Aganao Na Ibrahimu
Loading
/
Wagalatia 3:15-18

Hujambo msikilizaji wangu karibu sana tujifunze neno la mungu, leo twajifunza kwa undani fungu la neno nkutoka warakawa Paulo kwa Wagalatia 3:15-18, jina langu ni David mungai, wimbo alafu tuendlee

Naam katibu tena tujifunze neno, Wagalatia 3:15-18 ukweli wa agano na ibrahimu

Baba yetu ibrahimu ni mtu muhimu na wa maana katika mpango wa mungu kwetu na katika hitoria inayoonyesha namna mungu alidumisha uwepo wake kwa ibrahimu ni muhumu na tunayo sababu ya kujua na kufahamu ukweli wa agano katia ya mungu na ibrahimu. Hata yesu mwenyewe aliyazungumzia hayo katika vitabu vya injili.

Mtume Paulo pia aliwakumbusha wakorinho na warumi kuhusuagano hili sasa nasoma waraka wa Paulo kwa Wagalatia 3:15-18

15 Ndugu zangu, nanena kwa jinsi ya kibinadamu. Lijapokuwa ni agano la mwanadamu, hata hivyo likiisha kuthibitika, hakuna mtu alibatilishaye, wala kuliongeza neno.

16 Basi ahadi zilinenwa kwa Ibrahimu na kwa mzao wake. Hasemi, Kwa wazao, kana kwamba ni wengi, bali kana kwamba ni mmoja, Kwa mzao wako, yaani, Kristo.

17 Nisemalo ni hili; agano lililothibitishwa kwanza na Mungu, torati iliyotokea miaka mia nne na thelathini baadaye hailitangui, hata kuibatilisha ile ahadi.

18 Kwa maana urithi ukiwa kwa sheria, hauwi tena kwa ahadi; lakini Mungu alimkirimia Ibrahimu kwa njia ya ahadi.

Katika fungu hili la neno tunayo maneno Fulani yanayoonhyesha wazi ukweli halisi wa ahadi hii

Agano au makubaliano kati ya wawilihuonekana ahadi iliyopo ukitimia

Miaka mingi iliyo tangulia na kupita mungu aliwaahidi ibrahimubaraka kwa maneno haya, mwanzo12: 3

Name nitawabariki wakubariki naye akulaaniye nitamlaani na katika wewe jamaa zote zadunia watabarikiwa

Na katika mwanzo 17:4-5

Mimi agano langu nimefanya nawe nawe utakuwa baba wa mataifa mengi

Wala jina lako hutaitwa tena. Abrahamu litakuwa jina lako litakuwa ibrahimu kwani nimekuweka uwe baba wa mataifa mengi

Angalia kati ya mungu na ibrahimu lilifanywa na mwenyezi mungu mwenyewe miaka mingi sana kabla ya taifa la Israeli kuwepo n ahata torati halikuwepo Zaidi sana ibrahimu alikuwa mtu wa mataifa, taifa la Israeli lilikuwa bado kubuniwa

Ahadi hizi na agano lile lilikuwa naye mwenyei mungu katika mpango wake tangu

Mbegu ya kuongezeka kwafamilia lilitimizwa katika kristo yesu mesiya

Torati nayo iliyokuja kwa mkono wa Musa aliweka muhuri agano lile kwa kuja kwake yesu ke=risto bwana wetu maana ni Yesu kristo aliyeweka sharia yote kikamilifu kuwa basi tukitubu dhambi na kuungama na kughairi mienendo yetu na kumpokea yesu mioyoni mwetu basi katika jina la utukufu na lenye nguvu la yesu sisi basihuhusishwa katika agano na ahadi ile na tuna kuwa warithi wa zile ahadi na kujitwallia uzima na uzima wa milele wokovu katika yesu kristo ndiyo nguzo ya wokovu wetu

Receive Weekly Encouragement

Sign-up to get a sermon straight to your inbox on a weekly basis!