Uatili Wa Kihistoria

hft swahili 2022
Hope for Today (Swahili)
Uatili Wa Kihistoria
Loading
/
Danieli 7:15-28

Hujambo na karibuni. Hiki ni kipindi cha matumaini na leo twalichambua …. La neon la Mungu chuo cha Nabii Daniel 7:15-28. “UKATILI WA KIHISTORIA” Jina langu ni David Mungai. Wimbo halafu tuendelee. Naam, karibu tena, tujifunze Neno pamoja. Chuo cha Nabii Daniel 7:15-28. Basi mimi Daniel. Roho yangu ilihuzunika mwilini mwangu na hayo maono ya kichwa changu yakanifadhaisha.

16 Nikamkaribia mmoja wa hao waliosimama karibu, nikamwuliza maana ya kweli ya hayo yote. Basi akaniambia, akanijulisha tafsiri ya mambo hayo.

17 Wanyama hao wakubwa walio wane ni wafalme wane wataotokea duniani.

18 Lakini watakatifu wake Aliye juu wataupokea ufalme, na kuumiliki huo ufalme milele, naam hata milele na milele. 

19 Kisha nilitaka kujua maana ya yule mnyama wa nee, aliyekua mbali na wenziwe wote, wenye kutisha sana, ambaye meno yake yalikuwa na chuma na makucha yake ya shaba, aliyekula, na kuvunja vipande vipande, na kuyakanyaga mabaki ya miguu yake,

20 na habari za zile pembe kumi zilizokuwa kichwani mwake, na ile pembe nyingine iliyozuka ambayo mbele yake zilianguka pembe tatu, yaani pembe ile yenye macho, na kanwa lililonena makuu ambayo kuonekana kwake kulikuwa hodari kuliko wenzake.

21 Nikakitazama na pembe iyo hiyo ilifanya vita na watakatifu, ikawashinda.

22 hata akaja huyo mzee wa siku, nao watakatifu wake Aliye juu wakapewa hukumu; na majira yakawadia watakatifu waumiliki ufalme.

23 Akanena hivi, Huyo mnyama wa nne atakuwa ni ufalme wa nne juu ya dunia, utakaokuwa mbali na falme zile zote, nao utakula dunia yote, na kuikanyaga, na kuivunja vipande vipande.

24 Na habari za zile pembe kumi, katika ufalme huo wataondoka wafalme kumi; na mwingine ataondoka baada ya hao; naye atakuwa mbali na hao wa kwanza; naye atawashusha wafalme watatu.

25 Naye atanena maneno kinyume chake Aliye juu, naye atawadhoofisha watakatifu wake Aliye juu; naye ataazimu kubadili majira na sheria; nao watatiwa mikononi mwake kwa wakati, na nyakati mbili, na nusu wakati.

26 Lakini hukumu itawekwa, nao watamwondolea mamlaka yake, kuipoteza na kuiangamiza, hata milele.

27 Na ufalme, na mamlaka, na ukuu wa ufalme, chini ya mbingu zote, watapewa watu wa watakatifu wake Aliye juu; ufalme wake ni ufalme wa milele, na wote wenye mamlaka watamtumikia na kumtii.

28 Huu ndio mwisho wa jambo lile. Nami, Danielii, fikira zangu zilinifadhaisha, na uso wangu ulinibadilika; lakini naliliweka jambo hilo moyoni mwangu.

Katika lungu hili la neon la Mungu, twaona vile Mungu anavyoangalia falme za dunia. Kumbuka ya kwamba Mungu ndiye mfalme wa wafalme nay a Mungu ndito kweli.

Ndoto hii Danieli alitoa miaka 14 kabla ya wapashia na waamedi kuushinda ufalme wa Babelonia, mnamo mwaka wa 553 kabla ya kuzaliwa Kristo.

Akaona samba katika ndoto ambayo ni mfalme wake mfalme Nebukadneza, na ufalme wake wa Babilonia. Huyu Simba ana mabawa ya tai, maana yake akili potovu, lakini alipewa akili za kibinadamu, maana angebadilishwa kwa wema baadaye.

Mnyama wa tatu ni chui, na mabawa manne, ni mfanowa ufalme wa kingiriki/kiyunani, uliyoushinda ufalme Pashia na Media.

Yule chui alionekana kuwa na mabawa, kwa sababu wapiga vita wa Kigiriki, walikuwa wepesi sana katika vita.

Mnyama wa nne, alikuwa mwenye kutisha, mwenye nguvu, mwenye uwezo mwingi na meno ya chuma, yaonyesha ufalme wa kivumi wenye nguvu nyingi za kivita, katika siku alizotawala, na pembe 10, zaonyesha utawala wa mataifa kumi wa mwisho katika nchi ua Europa, mahali ambapo utawala wa mpinga Kristo – umeonyeshwa na pembe ile dogo itakaotokea kutoka kwa utawala wa Europa, siku za mwisho. Dalili zaonyesha hayo yatatokea baadaye.

Mpinga Krosto, atajaribu, kwa miaka saba ya dhiki na hataweza. UKATIKI WA HISTORIA. Yesu ndiye mfalme wa wafalme. Na katika Kristo sisi ni Washindi.

Receive Weekly Encouragement

Sign-up to get a sermon straight to your inbox on a weekly basis!